Friday, June 8, 2018

Mkurugenzi Ahimiza Uwajibikaji Watumishi wa Umma


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai, Yohana Sintoo akisisitiza jambo wakati wa kikao kazi cha maafisa wa serikali za mitaa kwa ngazi ya kata na vijiji kilichofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri hiyo mapema Juni 8. (Picha na Gasper Mushi)


Na Adrian Lyapembile
HAI
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai, Yohana Sintoo amewataka watumishi wa umma kwenye halmashauri hiyo kutekeleza wajibu wao kwa weledi na kuzingatia kutoa huduma bora kwa wananchi kwenye maeneo yao.

DC Awaasa Wanufaika TASAF Kujiunga na Bima ya Afya


Mkuu wa Wilaya ya Hai; Onesmo Buswelu akizungumza na baadhi ya wananchi wanaonufaika na Mradi wa Kunusuru Kaya Masikini unaofadhiliwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) alipotembelea zoezi la kuhawilisha fedha kwenye Kijiji cha Tindigani. Kulia kwake ni Diwani wa Kata ya Kia; Yohana Laizer. (Picha zote na Adrian Lyapembile)



Na Adrian Lyapembile
HAI

MKUU wa wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, Onesmo Buswelu amewataka wananchi wanaonufaidika  fedha zinzotolewa na mfuko wa maendeleo ya jamii (TASAF) kwa ajili ya  kunusuru kaya masikini kutumia  sehemu ya fedha hizo na kujiunga na bima ya afya.

Serikali Yajipanga Kumaliza Mgogoro wa Muda Mrefu

Mkuu wa Wilaya ya Hai, Onesmo Buswelu akisisitiza jambo kwenye mkutano na wananchi wa kijiji cha Tindigani alipofika kujadili namna serikali itakavyomaliza mgogoro wa mipaka ya kiwanja cha ndege cha KIA.   (Picha zote na Adrian Lyapembile)


Na Adrian Lyapembile
HAI

SERIKALI wilayani Hai, mkoani Kilimanjaro imesema mgogoro kati ya wananchi wanaopakana na  kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Kilimanjaro (KIA) utatuzi wake utazingatia sheria  na kila mwananchi haki yake italindwa kwa mujibu wa sheria  za nchi.

Thursday, May 24, 2018

Mamlaka Zatakiwa Kuzingatia Sheria ya Maji

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji Mhandisi Emmanuel Kalobelo (katikati) akisisitiza jambo wakati wa kikao chake na viongozi wa mamlaka za maji pamoja na viongozi wa Serikali katika wilaya za Hai na Siha mkoani Kilimanjaro. (Picha na Adrian Lyapembile)



Na Adrian Lyapembile
Hai

Mamlaka zinazojuhusisha na huduma ya maji kwa jamii imetakiwa kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia sheria ya Maji namba 12 ya mwaka 2009 inayoeleza wazi namna ya kushirikiana kati ya wahusika wakuu wa huduma hiyo ikiwemo serikali na vyombo vingine.

Wednesday, May 23, 2018

Watanzania Watakiwa Kuiunga Mkono Serikali


Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali Dk. Hasani Abbas (Mwenye miwani kulia) akisisitiza jambo alopofanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Yohana Sintoo wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua utendaji kazi wa Maafisa Habari na Mawasiliano wa Halmashuri pamoja na kufahamu changamoto wanazokutana nazo. (Picha na Adrian Lyapembile)

Na. Adrian Lyapembile

HAI


Watanzania wametakiwa kuiunga mkono serikali katika juhudi zake za kuwaletea maendeleo kwenye maeneo yao kwa kushiriki kulipa kodi mbalimbali zilizowekwa kisheria huku wakitambua kuwa kodi ni msingi wa maendeleo ya nchi hasa kwa wakati huu ambapo nchi inajizatiti kuelekea uchumi wa wa kati kwa kuimarisha viwanda.

Friday, May 18, 2018

Korosho kuimarisha Uchumi Wilaya ya Hai

Katibu Tawala Wilaya ya HAi Upendo Wella (aliyevaa miwani na skafu nyeusi) akiwaongoza viongozi wa ngazi mbalimbali kulipokea zao la korosho na kuinua juu miche ya zao hilo kama ishara ya kuinua uchumi katika Wilaya ya Hai (Picha zote na Praygod Munisi)

Na. Adrian Lyapembile
HAI

Wananchi wa wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro wametakiwa kuchangamkia fursa za kiuchumi kwa kushiriki kwenye kilimo cha mazao ya biashara likiwemo zao la korosho ambalo linastahimili hali ukame na kustawi kwenye mazingira ya ukanda wa tambarare wa Wilaya hiyo.

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye Kipindi cha Siku Mpya kinachurushwa na Redio Boma Hai 89.3 FM. 
(Picha na Adrian Lyapembile)

Na Gasper Mushi
HAI
Wito umetolewa kwa wapanda pikipiki mkoa wa Kilimanjaro kuvaa kofia ngumu (Helmet) wanapotumia vyombo hivyo vya moto ili kujilinda na kufuata sheria za usalama barabarani.

Monday, April 30, 2018

Walimu 146 Wahitimu Mafunzo ya Awali ya Skauti Wilaya ya Hai


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Edward Ntakiliho akisisitiza jambo wakati akizungumza na wahitimu wa mafunzo ya awali ya skauti kwa walimu wa shule za msingi na sekondari (hawapo pichani); hafla iliyfanyika kwenye ukumbi wa halmashauri hiyo tarehe 30/04/2018 (Picha zote na Adrian Lyapembile)


Na. Adrian Lyapembile
HAI

Wito umetolewa kwa walimu kuwa chachu ya tabia njema na mwenendo bora kwa kuishi maisha ya mfano kwa wanafunzi wao na jamii kwa ujumla katika kutekeleza majukumu ya kazi pamoja na kuwa wazalendo kwa kutanguliza mbele maslahi mapana ya taifa.

Saturday, April 28, 2018

DC Ahimiza Wazazi Kuwapeleka Watoto Kupata Chanjo za Magonjwa




Mkuu wa Wilaya ya Hai Onesmo Buswelu akifanya ishara ya uzinduzi wa chanjo ya Polio ya sindano kwa mmoja wa watoto waliofikishwa hospitali ya wilaya ya Hai leo Aprili 27, 2018 akishuhudiwa na wananchi na watumishi wa idara ya afya. 
(Picha zote na Adrian Lyapembile)

Na. Adrian Lyapembile

HAI


Mkuu wa Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro Onesmo Buswelu amewataka wazazi wilayani humo kuitikia mwito wa kuwapeleka watoto wao kupatiwa chanjo ili kuwakinga na magonjwa mbalimbali wanapofikisha umri wa kupatiwa chanjo hizo.

DC Aagiza Mto Sanya Usafishwe Kudhibiti Mafuriko


Mkuu wa Wilaya ya Hai Onesmo Buswelu (aliyevaa suti) akitoa maagizo kwa watendaji wa Halmashauri ya Wilaya kushirikiana na wananchi kurekebisha miundombinu ya Mto Sanya wakati wa ziara yake ya kukagua madhara yaliyosababishwa na mafuriko katika Kijiji cha Sanya Station mapema Aprili 19, 2018. (Picha na Davis Minja)


Na. Adrian Lyapembile
HAI

Mkuu wa Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro Mhe. Onesmo Buswelu amewaagiza wataalamu wa mazingira, kilimo na Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) kushirikiana kufanya usafi ndani ya mto Sanya eneo la Sanya Staion kuondoa mlundikano wa mchanga kwenye kina cha mto huo pamoja na kupanda miti na makingamaji kwenye eneo la mto alipofanya ziara ya kukagua madhara yaliyosababishwa mvua zinazoendelea kunyesha na kufanya mto kuacha njia ya asili na kuanzisha mkondo mwingine.

Friday, April 6, 2018

Wananchi Watakiwa Kutunza Miti Wanayootesha


Mkuu wa Wilaya ya Hai, Onesmo Buswelu akipanda mti kuashiria uzinduzi wa wiki ya kupanda miti uliofanyika Kijiji cha Mtakuja tarehe 05 Aprili 2018.
(Picha zote na Adrian Lyapembile)

Na Hellen Shayo
HAI

MKUU wa wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro, Onesmo Buswelu amewataka wananchi kutunza miti inayooteshwa katika kipindi hiki cha mvua ili iweze kukua na kukabiliana na hali ya ukame kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini.

Thursday, March 1, 2018

NAIBU WAZIRI MABULA AAGIZA WADAIWA SUGU KODI YA ARDHI WALIPE


Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Anjelina Mabula akisalimiana na mwenyeji wake Mkuu wa Wilaya ya Hai Onesmo Buswelu alipowasili kwenye ziara ya kikazi katika Wilaya ya Hai.


Na. Davis Minja
HAI

Naibu Waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi Anjelina Mabula ameitaka idara ya ardhi Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro, kutowafumbia macho wadaiwa sugu waliogoma au kuchelewa kulipia kodi ya ardhi wanazomiliki.

Wednesday, February 21, 2018

WALIMU WANOLEWA KUTUNZA MLIMA KILIMANJARO


Afisa maliasili Wilaya ya Hai Mbayani Mollel akitoa mafunzo juu ya mazingira kwa waalimu wa mazingira kutoka shule 25 wilayani Hai. (picha zote na praygod Munisi)

Monday, February 12, 2018

AFISA ELIMU AAGIZA KUANZISHWA JUKWAA LA WAZAZI SHULENI


Afisa Elimu Sekondari Wilaya ya Hai Julius Kakyama akisisitiza jambo kwenye kikao cha wazazi wa wanafunzi kwenye shule ya sekondari Hai. (Picha zote na Praygod Munisi)


Na. Praygod Munisi
HAI

Wakuu washule za sekondari za serikali katika wilaya  ya  Hai mkoani Kilimanjaro wametakiwa kuanzisha jukwaa la wazazi na walimu ndani ya mwezi mmoja ikiwa ni sehemu ya kutekeleza majukumu yao ili kutoa nafasi ya kujadiliana mambo mbalimbali kuhusu maendeleo ya shule na wanafunzi.

Wednesday, January 3, 2018

HAI YAPONGEZWA KWA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA AFYA


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo akikagua miradi ya maendeleo katika hospitali ya wilaya ya Hai alipofanya ziara ya kikazi. Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Anna Mghwira na kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wilaya ya Hai Yohana Sintoo. (Picha na Omary Mlekwa)


Na. Adrian Lyapembile
HAI


WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jaffo ameipongeza halmashauri ya wilaya ya hai kwa kuendelea kuboresha miundombinu katika hospitali ya wilaya hiyo itakayofanikisha kutekeleza azma ya serikali kutoa huduma bora za afya kwa wananchi wake.

Monday, December 11, 2017

NAIBU WAZIRI APONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI WILAYA YA HAI

Jengo la Bweni la Wanafunzi kwenye Shule ya Sekondari Harambee katika Wilaya ya Hai

Na. Riziki Lesuya
HAI


Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI George Kakunda amefurahishwa na kuridhishwa na usimamizi wa miradi ya maendeleo Wilayani Hai na kumpongeza Mkurugenzi Mtendaji  Yohana Sintoo  kwa usimamizi mzuri unaoendana  na thamani ya fedha iliyotumika.

MAREKEBISHO YA SHERIA KUTOKOMEZA MIMBA ZA UTOTONI

Naibu Waziri George Kakunda akizungumza na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Harambee alipofanya ziara ya siku moja katika Wilaya ya Hai.


Na. Adrian Lyapembile
HAI

Serikali imejipanga kufanya marekebisho ya sheria ya makosa ya kujamiiana ya mwaka 1998 ili kukabiliana na ongezeko la matukio ya  mimba kwa watoto walio chini ya miaka 18 hasa wanafunzi.