Na Adrian Lyapembile
HAI
Mkurugenzi
Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai, Yohana Sintoo amewataka watumishi wa
umma kwenye halmashauri hiyo kutekeleza wajibu wao kwa weledi na kuzingatia
kutoa huduma bora kwa wananchi kwenye maeneo yao.
Sintoo
ametoa rai hiyo kwenye mapema leo katika ukumbi wa halmashauri hiyo kwenye
kikao kazi cha siku moja cha watendaji wa serikali wa kada mbalimbali kwenye ngazi
ya kata na vijiji kilichokuwa na lengo la kuwakubusha utaakelezaji wa majukumu
yao na kuboresha huduma kwa wananchi.
“Baadhi
ya watendaji wamekuwa na tabia za kukwepa majukumu yako , ya kutatua kero za
wananchi na kugeuka kuwa sehemu ya migogoro kwa kuwapendelea baadhi ya watu ”amesema
Sintoo.
“Watendaji
wa kata hakikisheni kuwa mnasimamia watendaji wa vijiji pamoja na wataalamu
wote waliopo kwenye maeneo yenu ya
utawala ili wawajibike na kuhudumia wananchi
kwa kiwango kinachostahili ikiwemo kuondoa migogoro inayojitokeza kwenye
jamii” amesisitiza Sintoo.
“Wapo
watendaji miongoni mwenu wamekuwa na tabia za kufungua ofisi asubuhi na
kuondoka kwenda kwenye shughuli zao za
binafsi na kuwaacha wananchi wakipata shida pindi wanapohitaji huduma, tabia
hii sitaivumilia na wala sitasita kumchukulia hatua za kinidhamu yeyote atakayebainika
”ameongeza.
Akizungumzia
suala la baadhi ya wenyeviti wa mitaa na
vijiji kuigiza siasa katika shughuli za kimaendeleo, Sintoo amesema tabia hii imechangia
kuchelewesha upatikanaji wa huduma za kijamii kutokana na kuwagawa wananchi kwa
itikadi za kisiasa.
“Niwaombe
wenyeviti kuepuka kuingiza siasa kwenye utekelezaji wa shughuli za maendeleo na
mfahamu kuwa utekelezaji wa kazi za serikali hauzingatii upendeleo wa aina
yoyote au itikadi ya chama chochote kwani maendeleo hayana chama” ameongeza Sintoo.
Kwa upande wake mwanasheria
wa Halmashauri hiyo, Boniface Kalokona amewataka
watumishi kuacha tabia za kufanya kazi kwa woga ili kukwepa lawama na badala
yake wafanye kazi kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni zilizopo ambazo
hazipendelei wala kumuonea mtu yeyote bali zinatoa haki sawa kwa wote.
Naye mratibu elimu
kata ya Weruweru Angelika Kesi amesema
kikao hicho kimewakumbusha majukumu yao
pamoja na kupata njia za kuweza kutatua changamoto zinazijitokeza kwenye
maeneo yao hali ambayo itasaidia kuboresha huduma kwa wananchi.
Katika kikao kazi
hicho kilichowahusisha watendaji wa kata, watendaji wa vijiji, waratibu elimu
kata, maafisa maendeleo ya jamii kata pamoja na wakuu wa idara zao; kila
mtaalamu alipata nafasi ya kuzungumzia changamoto moja kwenye eneo lake la kazi
na namna ilivyotatuliwa lengo likiwa kutambua namna watendaji hao
wanavyowatumikia wananchi.
No comments:
Post a Comment