![]() |
Naibu Waziri George Kakunda akizungumza na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Harambee alipofanya ziara ya siku moja katika Wilaya ya Hai. |
Na. Adrian Lyapembile
HAI
Serikali
imejipanga kufanya marekebisho
ya sheria ya makosa ya kujamiiana ya mwaka 1998 ili kukabiliana na ongezeko la matukio ya mimba kwa watoto walio chini ya miaka 18 hasa wanafunzi.
Amesema
mabadiliko yatakayofanywa kwenye sheria hiyo ni pamoja na kuondoa dhamana kwa
watuhumiwa wa matukio ya ubakaji na waliowapa mimba wanafunzi lakini pia
washiriki katika kusababisha ndoa za utotoni ili kuepusha watuhumiwa kuharibu
ushahidi wa makosa waliyotenda pale wanapokuwa uraiani.
Aidha ameitaka
jamii kwa ujumla kushirikiana kupiga vita matukio ya mimba za utotoni na kwa wanafunzi ambayo yameonekana kuongezeka
kwenye mkoa wa Kilimanjaro na kubainisha kuwa wazazi wana mchango mkubwa katika
kutokomeza matukio hayo kwani ni kesi chache zinazofikishwa mahakamani na
nyingi hazitolewi hukumu kwa kukosekana ushahidi.
Amewataka walimu
na watumishi wa umma kuwa mabalozi wa kuwaelimisha wazazi kuhusu malezi ya
watoto na zaidi kujiepusha na namna yoyote ya ushiriki kwenye kuharibu ushahidi
pale inapotokea mtoto amepewa mimba bali washiriki kuhakikisha haki inatendeka
na wahalifu wanapata adhabu wanayostahili.
Wakati
huohuo Naibu Waziri Kakunda amewataka watumishi wa umma kuunga mkono juhudi za
Rais John Magufuli za kutunza rasilimali za nchi kwa kudhibiti matumizi ya
fedha hasa kwenye ujenzi kwa kutumia wataalamu waliopo kwenye maeneo yao kwa
mtindo wa ‘force account’ ambao umeonesha kuwa bora zaidi kwa miradi midogo ya
ujenzi.
No comments:
Post a Comment