Wednesday, February 21, 2018

WALIMU WANOLEWA KUTUNZA MLIMA KILIMANJARO


Afisa maliasili Wilaya ya Hai Mbayani Mollel akitoa mafunzo juu ya mazingira kwa waalimu wa mazingira kutoka shule 25 wilayani Hai. (picha zote na praygod Munisi)







Mtaalamu wa kilimo Wilaya ya Hai Simon Bunda akitoa maelezo wakati wa warsha ya mafunzo ya uhifadhi mlima Kilimanjaro kwa waalimu wamazingira kutoka shule 25 wilayani Hai.



Afisa mazingira wilaya ya Hai  Alfred Njegite akitoa maelezo wakati wa warsha ya mafunzo ya uhifadhi mlima Kilimanjaro kwa waalimu wamazingira kutoka shule 25 wilayani Hai.





Baadhi ya Waalimu kutoka katika shule 25 walayani Hai wakifuatilia kwa makini mafunzo ambayo yanahusu utunzaji wa mazingira yaliyo tolewa katika warsha ya siku moja na wataalam wanaohusika na mazingira.



Na Praygod Munisi na Davis Minja
HAI

Imeelezwa kuwa jamii ya watu wanaoishi karibu na hifadhi ya mlima Kilimanjaro wanao wajibu mkubwa wa kusaidia kutunza mlima Kilimanjaro ili kuendelea kupata faida na huduma zitokanazo na mlima huo.

Hayo yamebainishwa na Afisa maliasili wa Wilaya ya Hai Mbayani Mollel wakati wa warsha ya mafunzo ya siku moja ya uhifadhi wa mlima Kilimanjaro kwa walimu wa mazingira kutoka shule 25 za msingi pamoja na waratibu elimu kata.

Amesema kuwa kwa sasa bado kuna uhitaji mkubwa kwa jamii zilizozunguka mlima huo kuweka nguvu kwa kushirikiana na klabu za mazingira zilizopo shuleni ili kuweka msisitizo kwa wanafunzi kuwa na chachu ya kuhifadhi mazingira.

Mollel ameongeza kuwa zipo changamoto mbalimbali zinazo kabili uhifadhi wa mazingira ikiwa ni pamoja na,uvamizi wa misitu kwaajili ya kilimo,kuchoma misitu,kuingiza mifugo katika hifadhi ya misitu pamoja na ukataji miti kiholela jambo ambalo limekuwa likitishia hali ya uhifadhi wa mazingira.

Kwa upande wake Mgeni rasmi katika uzinduzi wa warsha hiyo Kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Hai Edward Mtakiliho amepongeza jitihada zinazo endelea kufanywa na walimu wa mazingira katika shule 25 zinazo zunguka mlima huo ambazo zimeonesha jitihada chanya za barafu ya mlima kilimanjaro kuongezeka au kubakia katika hali ya matumaini ya kuongezeka.

Ameongeza kuwa ikiwa jamii yote pasipo kutegemea uhifadhi huo kufanywa na wanafunzi au shule hali ya mazingira inaweza kuboreshwa kwa miasi ,ikubwa na kuzidi kuleta mafanikio zaidi.

Naye Rais wa Rotary klabu ya machame Raymond Uronu ameitaka serikali kuongeza nguvu katika makali ya sheria zinazo tumika kusimamia mazingira ili sheria hizo ziweze kufanya kazi kama ilivyo kusudiwa.

Uharibifu wa misitu Tanzania kwa mwaka ni Hekta 372,000 ambapo ni uvunaji haramu, moto, uvamizi mipaka,huku Mahitaji ya ujazo wa miti ni M3 milioni 62.3 na kilichopo ni M3 milioni 42.8 hivyo upungufu ni M3 milioni 19.5 kwa ajili ya matumizi. Upungufu huu wa mahitaji ni kichocheo cha uvunaji haramu wa misitu na kusababisha uharibifu wa vyanzo vya maji na upotevu wa misitu na ongezeko la hewa ukaa.






No comments:

Post a Comment