Zaidi ya
vijiji 11 wilayani Hai mkoani Kilimanjaro vikiwemo vijiji vya Mungushi,
Mtakuja, Tindigani na Mlima shabaha vinatarajia kunufaika na huduma ya umeme kupitia wakala wa umeme
vijijini REA huku vijiji vitakavyofuatia mara baada ya kukamilika kwa awamu
hiyo ni vijiji vya chemka, kambi ya nyuki, kilimambogo, mbatakero,pamoja na
modio.
Hayo
yamebainishwa na meneja wa
Tanesco Wilaya ya Hai Bw. James Chinula wakati wa uwasilishaji wa mada
katika kikao cha baraza la wafanyabiashara wilaya ya Hai
Chinula
amesema kuwa baada ya kupatikana kwa substation mpya ya KIA na kukidhi mahitaji
ya Wilaya ya Hai zaidi ya vijiji 11 vitapatiwa huduma hiyo kwa awamu ya kwanza.
Naye meneja
wa TRA Wilaya ya Hai na Siha bw. Silver Rutagwelera amesema kuwa katika mwaka
wa fedha 2013/2014 zaidi ya shilingi billion 1.7 zimekusanywa kama mapato huku
lengo la mwaka unaoanza ni kukusanya shilingi billion 2.2.
katika hatua nyingine wafanyabiasha bw. Johnson Mtey
amesema kuwa elimu ya matumizi sahihi ya mashine za EFD itolewe ili
kuondoa dhana iliyopo miongoni mwa wafanyabiashara juu ya matumizi ya mashine
hizo jambo ambalo bw. Rutagwelera amesema kuwa mbali na semina zilizotolewa
bado elimu zaidi inaendelea kutolewa.
Awali
akifungua kikao hicho Mkuu wa Wilaya ya Hai ndugu Novatus Makunga ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa baraza hilo
amesema kikao hicho ambacho sasa kitakuwa kinafanyika mara kwa mara kimelenga
kujadili fursa na changamoto za biashara zilizopo kwa lengo la kuimarisha na
kukuza biashara na kuongeza ushirikiano baina ya sekta binafsi na sekta za Umma
ili kuongeza ufanisi katika kazi.
habari imeandikwa na Gasper Mushi
habari imeandikwa na Gasper Mushi
No comments:
Post a Comment