Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Anjelina Mabula akisalimiana na mwenyeji wake Mkuu wa Wilaya ya Hai Onesmo Buswelu alipowasili kwenye ziara ya kikazi katika Wilaya ya Hai. |
Na. Davis Minja
HAI
Naibu
Waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi Anjelina Mabula ameitaka idara ya
ardhi Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro, kutowafumbia macho wadaiwa sugu waliogoma
au kuchelewa kulipia kodi ya ardhi wanazomiliki.
Mabula
amesema kuwa kumekuwepo na changamoto ya
watu kumiliki viwanja huku wakikataa kuvipima na kuchukua hati jambo linaloleta migogoro mingi katika maeneo
yao huku serikali ikipoteza kodi ya ardhi hivyo ni vema kufika mwisho wa kuwavumilia.
Mabula
ameongeza kuwa Wizara ya ardhi inapoelekea katika bajeti itaenda kubadilisha baadhi ya taratibu ili kuweza kuvitambua
viwanja ambavyo havijapimwa ili kubadilisha sheria na kuweka sheria itakayo
mbana mmiliki kulipa na kuepuka wananchi kuibia serikali kodi, na kuondoa changamoto
hiyo.
Aidha
amesema kuwa wizara imejaribu kutoa vitendea kazi vitakavyosaidia kutunza
kumbukumbu, kutambua wadaiwa na njia ya wao kufanya kazi kwa ufanisi, hivyo
asingependa kusikia kuwa vitendea kazi hivyo vimeshindwa kufanyakazi kwa
kutegemea wizara kukarabati au kuleta vipya, jambo ambalo ni kinyume kwani
halmashauri ndio inayotakiwa kuendelea kuhudumia vifaa hivyo kwa kutenga fungu.
Awali
akisoma ripoti ya utekelezaji wa ukusanyaji wa kodi ya ardhi kwa njia ya mfumo
wa kisasa uliowekwa na Wizara; Kaimu Mkuu wa Idara ya ardhi Jacob Muhumba
ametaja changamoto zilizopo za utumizi wa mfumo huo kufanyakazi taratibu sana
kutokana na tatizo la mtandao.
Katika
kutatua changamoto hiyo wamelazimika kutoa taarifa kwa katibu mkuu wizara ya
ardhi hivyo kuamini kuwa changamoto hiyo itatatulika na kuendelea kutoa huduma
hiyo kama ilivyokusudiwa.
Katika
kuzungumzia migogoro ya ardhi ndani ya Wilaya ya Hai Jacob amesema kuwa
migogoro ni ya kawaida huku mgogoro mkubwa ukiwa ni wa wananchi wa vijiji vya
sanya station, Tindigani na Chemka kutokana na baadhi ya kaya katika vijiji
hivyo kuingia katika eneo la uwanja wa Ndege jambo ambalo bado linashughulikiwa
na ofisi ya waziri Mkuu pamoja na TAMISEMI.
No comments:
Post a Comment