Friday, January 20, 2017

DC HAI ASITISHA KILIMO KWENYE SHAMBA LA FREEMAN MBOWE



Eneo linalotumiwa na Mh. Freeman Mbowe kwa shughuli za kilimo (Kilimanjaro Veggies)


Eneo linalotumiwa na Mh. Freeman Mbowe kwa shughuli za kilimo (Kilimanjaro Veggies)

Sehemu ya eneo la shughuli za kilimo katika shamba la Kilimanjaro Veggie

Mkuu wa Wilaya ya Hai Gellasius Byakanwa akitoa maelekezo ya serikali kwa mmiliki wa shamba
 Na Davis J. Minja
 HAI - KILIMANJARO

MKUU wa wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Gellasius Byakanwa, amesitisha shughuli za kilimo katika shamba la Kilimanjaro Veggies linalomikiwa na Mbunge wa jimbo la Hai Freeman Mbowe kutokana na shamba hilo kuwa ndani ya chanzo cha maji ya mto Weruweru.

Byakanwa alitoa amri hiyo baada ya kutembelea shamba hilo lenye ukubwa za zaidi ya ekari  mbili lililoko kijiji cha Nshara na kukuta kumeanzishwa shughuli za kilimo  ndani ya  chanzo cha maji kinyume na sheria na kufanya uharibifu wa mazingira.

Alisema Mbunge huyo amefanya uharibifu wa mazingira kwa kuvuna miti ya asili bila kibali cha Mkuu wa Wilaya kulingana na maamuzi ya kamati ya Ushauri ya mkoa (RCC) pamoja na kuvuta maji kwa kutumia  mashine kinyume na kibali na taratibu za utumiaji wa maji ya mfereji.

Alifafanua kuwa mnamo Januari 10 mwaka huu, alifanya ziara katika shamba hilo baada ya kupata malalamiko kutoka kwa wananchi pamoja na Mamlaka ya bonde la maji Mto Pangani na kujionea hali halisi ambapo alimwandikia Mbowe barua ya wito wa kufika ofisi ya mkuu wa wilaya mnamo Januari 13 akiwa na vibali vinavyomruhusu kufanya shughuli za kibinadamu katika eneo hilo.

Akizungumza kuhusiana na shughuli za kilimo katika eneo hilo, Nelly Mbowe ambaye ni dada wa Mbunge Freeman Mbowe anayesimamia shughuli hizo amekiri kufikisha taarifa kwa mbunge kuhusiana na wito aliopewa na Mkuu wa Wilaya.

Kwa  upande wake mwenyekiti wa Kijjiji cha  Nshara  Emanueli Mbowe alisema shughuli za kilimo katika eneo hilo zilianza mwaka jana ambapo alielezwa kuwa Mbowe anataka kuendeleza kilimo katika sehemu hiyo na anavyo vibali vyote zinavyomruhusu kufanya  shughuli hiyo.

No comments:

Post a Comment