Na Adrian Lyapembile
Hai
Mamlaka
zinazojuhusisha na huduma ya maji kwa jamii imetakiwa kutekeleza majukumu yake
kwa kuzingatia sheria ya Maji namba 12 ya mwaka 2009 inayoeleza wazi namna ya
kushirikiana kati ya wahusika wakuu wa huduma hiyo ikiwemo serikali na vyombo
vingine.
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Mhandisi Emmanuel Kalobelo ametoa
agizo hilo kama mwongozo wa namna ya kushughulikia mambo yanayohusu huduma ya
maji kwenye ngazi ya wilaya na mkoa ikiwemo kufahamu majukumu na mipaka ya
wadau hao wakuu wa sekta ya maji.
Akizungumza
na wadau wa huduma ya maji safi na maji taka katika wilaya za Hai na Siha mkoani Kilimanjaro alipofanya
ziara ya kikazi kutembelea miradi ya
maji inayotekelezwa na wizara hiyo, amesema vyombo vinavyotoa huduma ya maji
vinatakiwa kuzingatia sheria na miongozo iliyowekwa na kusimamia lengo kuu la
kuwapatia huduma bora wananchi hasa kwa wakati huu ambapo nchi inapita kwenye
mageuzi ya uchumi.
Kalobelo ameziagiza bodi za maji kuhakikisha kuwa gharama za kuvuta maji nyumbani zinakuwa nafuu ili kila mwananchi aweze kuzimudu ili kuweza kufikia malengo ya taifa la upatikanaji wa maji kwa jamii.
Amefafanua
kuwa lengo la kuanzishwa kwa mamlaka za utoaji wa huduma za maji ni kuisaidia
serikali kufanikisha usambazaji wa huduma ya maji kwa wananchi kwa mujibu wa
sheria ya maji.
“Bodi
za maji zitaendesha shughuli zake kwa kufuata sheria za nchi na ili kuweza
kutoa huduma za maji ni lazima usajiliwe kwenye mamlaka zinazohusika ili kuweza
kupata eneo la kutolea huduma ya maji kwa jamii ya eneo husika ”alisema Mhandisi Kalobelo
Aidha, Mhandisi Kalobelo alibainisha kuwa bodi za maji zitasaidiana na serikali kuboresha miundombinu pamoja na kuhakikisha kuwa zinafungua milango yake kwa wakaguzi wa serikali ili kuweka uwazi wa namna bodi hizo zinavyojiendesha.
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri
ya Wilaya ya Hai, Yohana Sintoo amesema kuwa
amepokea agizo la Wizara la kuweka uelewa wa pamoja na kuhakikisha sheria za maji zinafuatwa na
huduma za maji zinaboreshwa kwa manufaa ya wananchi wote.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Siha, Verial Juwal amesema kuwa wilaya hiyo ina bodi tatu zinazohudumia wakazi zaidi 120,000 kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012 kwenye kata 17 za wilaya ambapo kwa sasa wananchi wanapata maji kwa asilimia 84.
Hata
hivyo Mwenyekiti wa Bodi ya Lyamungo-Umbwe Michael Mmasy amesema
kuwa wataendelea kushirikiana na serikali ili kuhakikisha kuwa huduma za
maji zinaboreshwa kwa kuwapatia huduma ya maji wananchi wote wanaofikiwa na mtandao wa maji.
No comments:
Post a Comment