Na
Adrian Lyapembile
HAI
SERIKALI wilayani Hai, mkoani
Kilimanjaro imesema mgogoro kati ya wananchi wanaopakana na kiwanja cha ndege cha kimataifa cha
Kilimanjaro (KIA) utatuzi wake utazingatia sheria na kila mwananchi haki yake italindwa kwa
mujibu wa sheria za nchi.
Akizungumza na
wananchi katika ziara yake kwenye vijiji
vitano vinavyohusika na mgogoro huo, Buswelu amewataka kuwa na subira wakati
huu ambapo serikali inaendelea kutafuta
suluhu ya kudumu ya mgogoro huo.
Buswelu amesema serikali itafanya kazi
ya kuweka alama za kutambua mipaka
halisi ya maeneo ya kiwanja hicho ili kuweza kuwatambua wananchi ambao watakuwa ndani ya eneo
linalomikiwa na kiwanja hicho kwa ajili ya kuendelea na hatua za ufumbuzi.
“Nchi yetu inaongozwa na kuheshimu
sheria. Utatuzi wa mgogoro huu utazingatia sheria na kila mwananchi afahamu
kuwa haki yake italindwa kwa mujibu wa sheria; kama mtu anayo haki ya kulipwa
basi atalipwa kwa mujibu wa sheria”alisema Buswelu
“Mgogoro huu wa wananchi wanaopakana na kiwanja hicho umedumu
kwa muda mrefu kiasi cha kuwepo hali ya sintofahamu miongoni mwa wananchi hao
hasa pale wanapotakiwa kusitisha uendelezaji wa maeneo yao kwa kuweka majengo
ya kudumu kama nyumba, zahanati, shule za kudumu hali ambayo imewafanya
wananchi kulalamikia serikali lakini kwa sasa tunatafuta ufumbuzi wa kudumu ni
vema mkawa na subira”alisisitiza Mkuu huyo wa wilaya.
Akizungumzia hatua ya serikali
kumaliza mgogoro afisa kutoka Wizara ujenzi, Mawasiliano na uchukuzi, sekta ya
viwanja vya ndege, Mhandisi Rogatus Matigira alisema zoezi la kupima maeneo ya
kiwanja na kuweka alama litasaidia kufahamu ukubwa wa tatizo na kufahamu idadi
ya wananchi walio ndani ya maeneo ya kiwanja cha ndege lakini pia itasaidia.
“Serikali baada ya kuwa na huu mgogoro
muda mrefu wa mipaka kati ya Uwanja wa KIA na wananchi wanaoishi maeneo ya
jirani; imeona iangalie ukubwa wa tatizo kwa kupima na kuweka alama ndipo
ifanye maamuzi huku ikitumia maeneo ya kia kama rejea itakayosaidia kujua
walioko ndani na nje ”.
Diwani wa Kata ya Kia, Yohana Laizer akichangia mada kwenye mkutano wa Mkuu wa Wilaya ya Hai walipokuwa wakijadili namna ya kumaliza mgogoro wa mipaka ya kiwanja cha ndege cha KIA. |
Kwa upande wake Diwani wa Kata ya
Kia,Yohana Laizer ameiomba serikali kutumia hekima na busara kutafuta namna ya
kunusuru maeneo ya wananchi huku akikumbusha kuwa vijiji vya vimesajiliwa kwa
mujibu wa sheria lakini pia wao kama wananchi hawana uwezo wa kuitunishia
serikali.
Vijiji vinavyohusika na mgogoro wa mipaka na
uwanja huo ni Chemka,Rundugai, Sanya Station, Tindigani na Mtakuja ambavyo vipo
katika kata ya Masama Rundugai na Kia.
Baadhi ya Wananchi wa Kijiji cha Tindigani Wilaya ya Hai Wakifuatilia mkutano wa Mkuu wa wa Wilaya hiyo |
No comments:
Post a Comment