Afisa Elimu Sekondari Wilaya ya Hai Julius Kakyama akisisitiza jambo kwenye kikao cha wazazi wa wanafunzi kwenye shule ya sekondari Hai. (Picha zote na Praygod Munisi) |
Na. Praygod Munisi
HAI
Wakuu
washule za sekondari za serikali katika wilaya
ya Hai mkoani Kilimanjaro
wametakiwa kuanzisha jukwaa la wazazi na walimu ndani ya mwezi mmoja ikiwa ni
sehemu ya kutekeleza majukumu yao ili kutoa nafasi ya kujadiliana mambo mbalimbali
kuhusu maendeleo ya shule na wanafunzi.
Agizo
hilo limetolewa na Afisa Elimu sekondari wilaya ya Hai Bw. Julius Kakyama
wakati akizungumza na wazazi katika kikao kilichofanyika katika shule ya sekondari
Hai iliyopo mjini Bomang’ombe, ambapo amesisitiza ushirikiano kwenye jukwaa la
wazazi na walimu na kuwataka kutumia jukwaa hilo kama sehemu sahihi ya kutatua
changamoto zinazowakuta wanafunzi katika safari yao ya kutafuta elimu.
Wazazi wakimsikiliza kwa Afisa Elimu Sekondari wilaya ya Hai Julius Kakyama (hayupo pichani) alipofanya kikao na wazazi wa wanafunzi kwenye shule ya sekondari Hai. (Picha na Praygod Munisi) |
Kakyama
amewakumbusha walimu kuwa na nidhamu na maadili ili wawe mfano mzuri wa kuigwa
na wanafunzi wanaowafundisha na hatimaye kutengeneza taifa lenye watu waaminifu
wenye nidhamu ambao watashiriki kikamilifu katika kuleta maendeleo ya taifa
lao.
Aidha
Kakyama amewakumbusha wazazi kusimamia vizuri jukumu lao la malezi kwa
wanafunzi wanapokuwa nyumbani kwa kufuatilia kwa karibu maendeleo ya masomo ya
watoto wao ikiwemo kuwapatia mahitaji yote muhimu kwa pamoja na kuhakikisha
kuwa wanahudhuria shuleni huku wakiwalea watoto hao katika maadili mema
wakishirikiana na walimu jambo ambalo litasaidia kupunguza changamoto za utoro mashuleni lakini pia itasaidia kuongezeka
kwa kiwango cha ufaulu.
Afisa
Elimu Sekondari anafanya mikutano ya mara kwa mara na walimu pamoja na wazazi
katika shule zilizopo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Hai ambapo amekuwa
akishiriki kujadili maendeleo ya elimu wilayani pamoja na kutoa tafsiri ya
maelekezo ya serikali ikiwemo kutambua nafasi ya mwalimu, mzazi na mwanafunzi
katika swala zima la elimu bila malipo.
No comments:
Post a Comment