TAARIFA YA MFUMO WA ULINZI KWA
MTOTO PAMOJA NA MAADHISHO WILAYA HAI ILIYOSOMWA NA MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA
WILAYA YA HAI NDUGU M.O.HUMBEKATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA NA
UZINDUZI WA KITUO CHA ONE STOP CENTER
NDUGU MGENI RASMI ; Mei 2010 Halmashauri ya Wilaya kwa kushirikiana na Idara ya Ustawi wa Jamii makao makuu na UNICEF Tanzania, ilifanya utafiti juu ya ulinzi kwa mtoto matokeo yalikuwa kama ifuatavyo.
• Kiwango cha
uelewa wa jamii juu ya ulinzi kwa mtoto ni mdogo sana.
• Mfumo na
muundo wa timu ya ulinzi kwa mtoto sio makini katika kupinga na kuitikia ukatili
dhidi ya kw a watoto.
• Idadi kubwa
ya makao ya kulea watoto na mengi
kuendeshwa chini ya kiwango .
NDUGU MGENI RASMI; Utafiti huu ulipelekea Wilaya
kuwa na mikakati ifuatayo;
• Kuunda timu
za ulinzi kwa mtoto
• Kupunguza
makao ya kulea watoto yatima na watoto wa mazingira hatarishi
• Kupinga na
kuitikia ukatili dhidi ya watoto.
NDUGU MGENI
RASMI; Baada ya utafiti Halmashauri
kwa kushirikiana na wadau ilibaini kuwa
mifumo iliyopo ya haina ushirikiano wa kutosha
katika kutoa huduma kwa watoto
waliofanyiwa ukatili ndipo
mkakati wa uundaji wa timu ya
ulinzi kwa mtoto kuanzia ngazi ya wilaya ,kata na vijiji uliundwa kwa kuzingatia
sekta zote zinzazohusika na ulinzi na usalama kwa mtoto wakiwemo,Maafisa ustawi wa jamii ,Mipango ,Hakimu mkazi (W),Wajumbe
kutoka baraza baraza la watoto, Polisi
dawati la jinsia na watoto& mwendesha mashtaka Afisa huduma kwa jamii, Afisa
maendeleo ya jamii, Mwanasheria Wilaya Afisa Elimu Sekondari ,Afisa elimu msingi , Madaktari
wawili na Afisa afya Wawakilishi wa wawili wa asasizisizo za serikali kutoka ( KIWAKUKI NA HANGO).
NDUGU MGENI RASMI;
Mafanikio yaliyopatikana baada ya kuanzisha mfumo wa ulinzi
kwa mtoto
• Kupunguza
makao ya watoto kutoka 22 hadi kufikia 7 kwa kufunga makao na kutoa mwongozo wa kitaifa ambayo yanaendeshawa chini ya kiwango ,
• Kuwaunganisha
watoto 179 na familia zao/jamii kutoka katika makao ya watoto yanayolea watoto yatima na
mazinhira magumu, watoa huduma
497 wa watoto wamepata mafunzo juu ya ulinzi
na usalama wa mtoto kisheria. (
walimu 342 ,manesi 40 ,polisi 76 ,
maafisa wa mahabusi ya watoto, makatibu wa baraza la kata, maafisa
magereza 2 and madiwani 2, Mahakimu 8 kutoka Mahakam ya
wilaya na mahakama ya mwanzo.
• Walezi( fit
person) 50 wa watoto waliofanyiwa ukatili wametambuliwa katika jamii,
• Kuwepo na
mfumo wa ukusanyaji wa taarifa za watoto walio fanyiwa ukatili (child
protection informationManagement system)
• Kuongezeka
kuripotiwa kwa matukio ya watoto waliofanyiwa ukatili na watu wazima
waliofanyiwa ukatili wa kijinsia kwa
sababu ya kuwepo na uelewa mkubwa katika jamii juu ya kupinga ukatili kwa
watoto na unyanyasaji wa kijinsia (Vionlence agaist children (VAC)& Gender
based violence (GBV) kutoka 59 mwaka 2009
hadi kufikia 3306 kwa mwaka 2013.
• Kuwepo na
ushirikiano mkubwa sana baina ya ofisi ya ustawi wa jamii ,dawati la na watoto jinsia,mahakama ,elimu, na
hospitali, kuwahudumia watoto na wadau wengine
• Watoto
kuweza kuripoti matukio ya ukatili
katika dawati la jinsia na watoto polisi na ustawi wa jamii.
• Kesi za
watoto kupewa kipaumbele katika mahakama.
• Kutolewa
kwa msaada wa dharura kwa watoto waliofanyiwa ukatili 275
• Watoto
330 wa mazingira magumu wamepatiwa vyeti
vya kuzaliwa
• Kuwepo na
kituo jumuishi cha kutoa cha kutoa huduma
za pamoja kwa watoto waliofanyiwa ukatili pamoja ukatili wa kijinsia (one stop
centre) ambacho kinahusisha watoa huduma watatu polisi,daktari na ustawi wa
jamii.
NDUGU MGENI RASMI; Changamoto
tunazokutana nazo katika kufanya shughuli za ulinzi kwa mtoto.
• Baadhi ya
mila na desturi ni kikwazo katika kutoa taarifa za ukatili kwa watoto kama vile ndoa za mapema
• Kukosa
ushirikiano kutoka kwa wanajamii katika utoaji wa ushahidi mahakamani hususa kesi za
ukatili wa kingono (kubaka ,kulawiti na unajisi)
NDUGU MGENI RASMI; Tunapenda kutoa shukrani
zetu za dhati kwa wadau waliotuwezesha kufika hapo tulipo ,UNICEF Tanzania,Save
the children Tanzania,Wizara ya Afya na ustawi wa jamii- idara ya
ustawi wa jamiii ,wizara ya mambo ya ndani idara ya polisi,wizara ya
wanawake jinsia na watoto na wizara ya
katiba na sheria - idara ya mahakama ,pamoja na asasi za kiaraia. NDUGU MGENI RASMI; Makakati wa wilaya
katika kupinga ukatili kwa watoto ni;
• Kutoa
huduma kwa umakini na weredi katika kituo jumuishi kwa watoto waliofanyiwa
ukatili na watu wazima walio fanyiwa ukatili wa kijinsia
• Kuelimisha
jamii kwa njia ya radio ,televisheni,shule za sekondari na msingi , taasisi za
kidini ,vyama vya kisiasa na mitandao mingine ya kijamii.
• Kuunda timu
katika kata 4 mpya na vijiji 5 vipya
• Kuendeleo
kuwaunganisha watoto katika jamii kutoka katika makao na wengine walio kitengana
na familia au jamii zao.
• Kuendelea
kufanya kazi kwa pamoja ili kuimarisha mfumo
na muundo wa ulinzi kwa mtoto uliopo.
• Kuwepo na
usafiri wa uhakika katika kuitikia na
kufuatilia matukio za ukatili kwa watoto
• Kuendelea
kutumia fursa zilizopo katika kutekeleza shughuli za ulinzi kwa mtoto.
NDUGU MGENI RASMI; Mwisho tunapenda kutoa wito
kwa Wilaya nyingine kuanzisha mfumo huu wa ulinzi na usalama ili kuweza kwa
mtoto ili kuweza kumlinda na kumjali mtoto wa Kitanzania.
No comments:
Post a Comment