HOTUBA YA KATIBU TAWALA MKOA NDUGU
FAISALI ISSA WAKATI WA UZINDUZI WA KITUO
CHA PAMOJA CHA KUTOA HUDUMA KWA WAATHIRIKA WA UKATILI WA KIJINSIA. IMESOMWA KWA
NIABA YAKE NA MHANDISI WA MAJI MKOA WA KILIMANJARO ALFRED SHAYO.
Ndugu Mkuu wa Wilaya ya Hai , Novatusa Makunga
Mh Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya hai,Clement Kwayu
Ndugu mwakilishi wa UNICEF Tanzania
Ndugu mwakilishi wa Serve the Children Tanzania
Ndugu Mwakilishi wa Kamishna- Polisi
Ndugu Mkurugenzi wa Watoto-Wizara ya Maendeleo ya Jamii
Ndugu Wawakilishi wa asasi za kiraia,Madhehebu na Dini
Viongozi wote ,mabibi na mabwana
Awali ya yote nimefarijika kupata nafasi hii muhimu ya
kushuhudia uzinduzi wa kituo cha pamoja cha kutolea huduma kwa waathirika wa
Ukatili wa kijinsia hasa watoto.
Ni matumaini yangu kwamba uzinduzi wa kituo hiki utakuwa
chachu ya kutolewa kwa taarifa za ukatili wa kijinsia hasa kwa watoto baada ya
upatikanaji wa huduma hizo kurahisishwa.
Ndugu wananchi, kituo hiki kimezinduliwa siku ambayo pia ni
siku ya kuadhimisha siku ya Mtoto wa Afrika huku kauli mbiu ikiwa ni ”KUPATA
ELIMU BORA NA ISIYO NA VIKWAZO NI HAKI YA KILA MTOTO.” kutokana na kauli mbiu hii ni vema kila
mmoja wetu kwa kutumia nafasi aliyo nayo atimize wajibu wake ili kuhakikisha
mtoto anapata haki yake ya msingi ya elimu bora.
Tumieni fursa iliyopatikana ya kituo cha pamoja kwa ajli ya
kutoa taarifa za ukatili kwa watoto,ukatili ambao wakati mwingine
unamsababishia mtoto kukosa fursa ya Elimu.
Acheni tabia ya kumaliza masuala ya ukatili wa kijinsia
katika ngazi ya familia kwakufanya hivyo
kamwe hamtaweza kutokomeza matukio haya.
Tunajua kuwa wakati mwingine inakuwa ni vigumu kwa wanandugu
kufikishana katika vyombo vya sheria ili kutovunja undugu, lakini tukiendelea
kuwafumbua macho hawa watu eti kwasababu ni ndugu matukio kama haya yataisha,
sasa je mtoto atapata haki yake ya msingi na kutimiza kauli mbiu ya mwaka huu?
Ni wakati wa mabadiliko na mabadiliko yanaanzia Katika Wilaya
ya Hai kwakutumia vema rasilimali zilizopo ambazo ni pamoja na Kituo Jumuishi
cha pamoja.
Mkuu wa Wilaya na pamoja na timu yako ya Wataalam,
Napenda kuwapongeza kwa mafanikio
mliyofikia baada kuanzisha mfumo wa ulinzi kwa mtoto na sasa kufikia hatua ya
kuwa na kituo hiki.Ni mafanikio ambayo jamii ya wanahai lazima
wajivunie.Naamini wakati umefika kwa
Wilaya zingine kuja kujifunza kutoka kwenu kwa mafanikio yaliyopatikana baada
ya kuanzisha mfumo wa ulinzi kwa mtoto
Katika taarifa zenu awali mmesema
mmefanikiwa kupunguza makao ya watoto kutoka 22 hadi 7, tumieni ujuzi na mbinu
mlizo tumia kupunguza makao hayo kusaidia Wilaya za jirani ambazo bado makao ya
watoto yanaonekana kama suluhu ya kusaidia watoto walio katika mazingira
hatarishi huku baadhi ya wenye makao hayo wakitumia kama njia ya kujinufaisha.
Ni
wazi kuwa kuongezeka kuripotiwa kwa matukio ya watoto waliofanyiwa ukatili na
watu wazima waliofanyiwa ukatili wa kijinsia umesababisha na elimu mliyoitoa katika jamii
ni vema mkaendelea kutoa elimu hiyo hasa kwakutumia vyombo vya habari.
Kufunguliwa
kwa kituo hiki iendeleze ushirikiano
uliopo kati ya ofisi ya ustawi wa jamii ,dawati la na watoto jinsia,mahakama ,elimu, na
hospitali, kuwahudumia watoto na wadau wengine
Ndugu wananchi,
Serikali
yetu inatoa shukrani kwa wafadhili
waliosaidina katika kufanikisha ujenzi wa kituo hiki ambao ni UNICEF Tanzania na
Save the children Tanzania. Fedha zilizotumika katika ujenzi wa kituo hiki
naamini hazijapotea bali zitaleta matunda mazuri. Tunaomba muendele kuisaidia
serikali katika kufikisha huduma kwa jamii. Serikali inatambua mchango wenu, na
inaahidi kusimamia vema michango yoyote ile mtakayoitoa.
Natoa
wito wito kwa wazazi,walezi na wadau wengine pamoja na viongozi wa ngazi zote
kuendelea kutoa taarifa za ukatili dhidi
ya watoto na ukatili mwingine wa kijinsia ili kuweza kuwa na Jamii ilivyostawi
na kuwa na maendeleao katika nchi.
No comments:
Post a Comment