Rai hiyo imetolewa
Afisa
Mkuu wa uhamiaji Mkoa wa
Kilimanjaro ndugu Johanes Msumule wakati wa kuwasilisha mada katika kikao cha baraza la biashara Wilaya ya Hai
ambacho kimehudhuriwa na wadau mbalimbali wa biashara pamoja na wakuu wa idara.
Msumule
amesema kuwa elimu zaidi inaendelea
kutolewa kwa wananchi kwani wengi wao wamejikuta wakitahifishiwa mali zao au kutumikia adhabu mbali mbali pale ambapo
wanawafadhili au kuwahifadhi wahamiaji haramu kitendo ambacho ni kinyume na
sheria.
Naye Afisa Habari
wa Wilaya ya Hai Bi. Rizik Lesuya
ameushauri uongozi wa idara ya uhamiaji kutumia vyombo vya habari kama
vile radio, Tv pamoja na magazeti ili kutoa
elimu hiyo kwa wananchi wengi zaidi .
Naye Janesta Urio kutoka kutoka sido Kilimanjaro amesema
kuwa ili kutoa mwanya zaidi kwa wananchi kutoa taarifa juu ya matukio ya
uhalifu viongozi hawana budi kufuata maadili ya kazi yao ikiwemo kumwifadhi
mtoa taarifa ili asidhurike kwa namna yeyote ile pale anapotoa taarifa juu ya
vitendo vya uhalifu.
Katika hatua
nyingine Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Hai ndugu Zabriel Moshi
amewashukuru washiriki wa kikao hicho sambamba na kuahidi kuzifanyia kazi
changamoto zilizoelekezwa katika ofisi yake likiwemo suala la ukarabati wa choo
cha soko la walaji Hai mjini
habari hii imeandikwa
Na Edwin Lamtey
Na Edwin Lamtey
No comments:
Post a Comment