Thursday, May 22, 2014

MABADILIKO YA TABIA NCHI YAADHIRI UCHANGIAJIA WA MIRADI



IMEELEZWA kuwa kutokamilika kwa wakati kwa  miradi ya kimaendeleo  imechangiwa na baadhi wa wanajamii kushindwa kuchangia  kutokana na mabadiliko ya tabia nchi

Hayo yamelezwa na Diwani  Kata wa Masama Rundugai Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro , Mh Fadhili Juma  wakati akiwsilisha taarifa ya hali ya utekeleza wa miradi ya kimaendeleo katika kikao  cha baraza la madiwani kilichofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri ya Hai  

Amesema  mabadailiko ya tabia nchi  yaliyotokea yamepelekea uchumi wa wananchi kuyumba kutokana na kutopata mavuno ya kutosha katika msimu uliopita hali iliyosababisha wananchi wengi kukumbwa na nja na kushindwa kutoa michango kwani kata hiyo wananchi wengi hutegemea Kilimo 

Kwa upande wake Mh Diwani wa Kata ya Machame Weruweru, Mh Adris Mandrai  akitoa taarifa ya hali ya utekezaji wa robo ya  tatu  alisema kuwa miradi inayotekelezwa katika Kata hiyo imeendelea vizuri ila michango ya wananchi   imekuwa ya kususua jambo ambalo limesababisha miradi kukwama.

Alisema mabadiliko ya tabia nchini imepelekea  baadhi ya maeneo ya Kata hiyo kuwa katika hatari ya kukumbwa na baa la njaa endapo mvua za masika zitaisha mapema.
Mh Mandrai amesema   kuwa vijiji vilivyopo katika hatari ya kukumbwa na baa la njaa ni vijiji vya Ngosero na Minjongweni ambapo amefafanua kuwa pamoja na jamii  wananchi kulima kwa wingi bado tatizo la mabadiliko ya tabia nchi yamendelea kuathiri kutokana na kukoseka kwa mvua za masika.

Naye Diwani wa Kata ya Masama Kati, mh Deogratus Kimaro akiwasilisha taarifa katika kikao cha baraza hilo amesema kuwa   baadhi ya viongozi wa vijiji wamekwamisha miradi ya kimaendeleo kutokana na kushindwa  kuitisha  vikao vya kisheria .

Kufuati  hali hiyo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai,Mh  Clement Kwayu aliagiza watendaji  wa vijiji  ambao wameshindwa  kusoma mapato na matumizi kwa muda mrefu kuandaa taarifa hizo na kuzifikisha katika Ofisi ya Mkurugrnzi mapema wiki ijayo na baada ya hapo waitishe vikao na kutaka kwa atakayeshindwa kutekeleza agizo hilo achukuliwe  hatua za kinidhamu.

Kufuatia hilo Baraza la Madiwani pia limewataka wataalamu kutembelea vijiji ambavyo vimekuwa na migogoro ili kuweza kutatua matatizo ambayo yamekuwa yakikwamisha kuendelea kwa shughuli za kimaendeleo katika jamii .

Akichangia katika kikao hicho, Mkuu wa Wilaya hiyo, Novatus Makunga  amemtaka Mkurugenzi  Mtendaji  kuwachukulia hatua ya kinidhamu  watumishi  wanaoshindwa kutekeleza majukumu yao jambo ambalo ni changamoto katika kuteleza shughuli za kimaendeleo





Aliyesimama wa kwanza kutoka Kulia ni  Diwani wa Kata ya Masama Mashariki mh  Twalibu  Mwanga akitoa taarifa ya robo ya tatu ya kata yake 'Usalama na ulinzi kwa kata yetu ni nzuri licha ya matukio yaliyojitokeza,tunaishukuru Jeshi la Polisi Wilaya ya Hai kwa Ushirikiano wao' ni sehemu ya taarifa ya Mh Mwanga Wakati akiwasilisha taarifa ya Kata yake wakati wa Baraza la Halmashauri lililofanyika Jana.




  
Mh Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai na Diwani wa kata ya Kata ya Machame Kaskazini Clement Kwayu akiwasilisha taarifa ya Robo ya tatu ya kata yake.



 Diwani wa kata ya Masama Kusini  aliyesimama wakwanza kulia Mh Issa Kiasnga akitoa taarifa ya robo ya tatu ya kata yake,alisisitiza juu ya matumizi ya dawa ya kulevya yanavyoathiri nguvu kazi na kuliomba Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na wananchi kuziba mianya ya usafirishaji wa madawa hayo hasa mirungi na bangi ambayo amesema katika Wilaya ya Hai hakuna eneo linalolima madawa hayo ya kulevya yalikini yamekuwa yakitumia na baadhi ya Vijana.




Aliyesimama wa kwanza kulia ni Diwani wa kata ya Machame Mashariki  Mh Rajabu Nkya akitoa taarifa ya kata yake 'ninaona fahari kwa kata yangu kuwa na Kaya nyingi zilizojiunga na Mfuko wa Bima wa Afya ya Jamii bado tunaendelea kuhamasisha wananchi wajiunge na mfuko huo.' 






Aliyesimama wa kwanza kulia ni Diwani wa kata ya Masama Kati Mh Deogratius Kimaro akitoa taarifa ya robo ya tatu ya Kata yake,'tupo katika mchakato wa kuboresha vituo vya afya na zahanati ili kufikisha huduma kwa wananchi kwa gharama ndogo'




Aliyesimama ni Diwani wa Kata ya Machame weruweru Mh Adris Mandrai akitoa taarifa katika Baraza la Halmashauri mapema jana "mikakati tuliyonayo katika kukamilisha miradi ya maendeleo ni pamoja na kutoanzisha miradi mipya kabla ya kukamilisha iliyopo,kutoa taarifa ya mapato na matumizi kwa wananchi na kuhamasisha uchangiaji miradi ya maendeleo'




Mh Fadhili Mchomvu Diwani wa Masama Rundugai akitoa taarifa ya Robo tatu ya  Kata yake.









Diwani wa kata ya Machame Kusini Mh Nasibu Mndeme akitoa taarifa ya robo ya tatu ya kata yake,"tunaendelea kuzuia utengenezaji wa pombe kwakutumia mahindi na kuzingatia kilimo bora ili kuepukana na uhaba wa chakula"
 















































No comments:

Post a Comment