Monday, May 26, 2014

MKUU WA WILAYA YA HAI AWATAKA VIONGOZI WA VIJIJI KUSIMAMIA SHERIA



Mkuu wa wilaya Hai, ndugu Novatus Makunga amewaagiza viongozi wa vijijji na vitongoji vinavyopitiwa na barabara ya Machine Tools hadi Machame kusimamia sheria ya barabara  ili kudhibiti uswagaji wa mifugo hususani ng’ombe katika barabara hiyo .

Mkuu huyo wa Wilaya ametoa agizo hilo baada ya kukagua barabara hiyo ambayo ilikarabatiwa kwa kipande cha kilometa 7.9 na Wakala wa barabara nchini, Tanroads na baadaye alikagua barabara nyingine ya Kwasadala hadi Masama inayoendelea kujengwa na wakala huyo.

Akizungumza na viongozi mbalimbali wa vijiji vya kata ya Machame Kaskazini ambapo barabara hiyo imepita,aliwaiwaagiza Watendaji hao kusimamia sheria inayozuia mifugo kutembezwa barabarani badala ya wao kama viongozi kuanza kulalamika.

Viongozi hao awali walimweleza Mkuu huyo wa Wilaya kwamba kwa asili ya eneo la Machame siyo la ufugaji wa mifugo inayochungwa bali ufugaji wao ni ule wa ndani, hata hivyo limezuka wimbi la wamiliki wa Mabucha kwenda minadani na kununua ng’ombe ambao katika kuwasafirisha uamua kuwachunga barabarani na hivyo kusababisha uharibifu wa barabara.

Kwa upande mwingine Makunga amemwagiza Kaimu meneja wa Wakala wa Barabara, Tanroads Mkoani Kilimanjaro Mhandisi Reginald Massawe kuandaa semina ya uelewa kwa viongozi wa vjiji na vitongoji itakayolenga kuwaelimisha juu ya sheria ya hifadhi ya barabara pamoja na mpango wa kuisimamia na kuwapa nakala ya sheria hiyo ili waanze kuitekeleza.

Pia amewataka viongozi hao kutoa notisi kwa wamiliki wa mabucha kuhusiana na kuanza utekelezaji wa sheria hiyo.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Wilaya amemtaka Mhandisi Massawe kutuma wataalamu watakaoianisha mapungufu mbalimbali ambayo yamejitokza katika ukarabati huo wa baabara yakiwemo ya baadhi ya maeneo kutokuwa na makalvati, mikondo ya maji kutokuelekezwa kwa usahihi, baadhi ya maeneo ya  lami kuanza kumeguka pamoja na mahitaji ya  kuweka alama za kuvuka kwa waenda kwa miguu.

Awali mhandsi Massawe ameeleza wakala wa barabara imetumia kiasi cha shilingi milioni 1,005 kukarabati sehemu ya kilometa 7.95 ya barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 14.98.Amesema kazi zilizofanyika ni pamoja na kuondoa tabaka la lami, kuvuruga msingi wa awali, kujenga msingi mpya nakuweka tabaka jipya la lami nyepesi kwa upana wa barabara wa mita 9.0.

Amesema kuwa dosari mbalimbali zilzojitokeza ambazo walizibaini katika ziara hiyo ya Mkuu wa Wilaya ambazo znahtaji fedha nyingi zitafanyiwa kazi katika awamu ijayo ya kukarabati barabara hiyo ambayo itaingizwa katika mwaka ujao wa fedha ambao unaanza mwezi.

Amesema kuwa katika mwaka ujao wa fedha kiasi cha shilingi milioni 800 zimetengwa kwa kazi ya kupanua mabega ya barabara kila upande na kujenga tabaka la lami nyepesi sehemu ya barabara yenye urefu wa kilometa 5

Akiwa  katika barabara ya Kwasadala hadi Masama mkuu huyo wa wilaya amemtaka Mkandarasi kushirikiana na viongozi wa eneo hilo katika kuhakikisha ujenzi wa makalvati ya kupitisha maji unakwenda kwa usahihi kwa lengo la kuepuesha madhara hasa nyakati za masika.

Aidha amemtaka Mkandarasi huyo kutatua tatizo la baadhi ya maeneo kushindwa kupitika kutokana mvua zinazonyesha sasa kwa kumwaga vifusi hasa katika maeneo yenye miteremko mikali.

Mkandarasi mpya wa barabara hiyo kampuni ya Hari Singh and Sons Limited ameahidi kurekebisha sehemu zote korofi katika kipindi hiki cha mvua wakati kazi ya ujenzi huo ambayo imefikia asilimi tano ikiwa inaendelea.

Mkandarasi huyo alianza kazi mwezi Januari mwaka huu baada ya kuvunjwa kwa mkataba wa Mkandarasi wa awali katika barabara hiyo ambayo ni ahadi ya rais Jakaya Kikwete.

Ujenzi wa barabara hiyo yenye urefu wa Kilometa 12.5 unatarajiwa kukamilika mwezi Januari Mwakani.


Mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga akipata ufafanuzi wa Ujenzi wa Barabara ya Machame kutoka kwa Kaimu Meneja wa Tanroads mkoani Kilimanjaro, Mhandisi Reginald Massawe(Kushoto)


Mwenyekiti wa kijiji cha Nshara akimwonyesha mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga pamoja na Maofisa wa Tanroads mkoani Kilimanjaro moja ya eneo hatari kwa watumia barabara ya Machame katika kona ya Lambo






Mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga na maofisa wa Tanroads wakishuhudia mifugo  ikisagwa katika barabara ya Machame



Mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga akitoa maelekezo ya barabara ya Machame,kulia ni mmoja ya wataalamu wa ujenzi katika wilaya ya Hai,Mhandisi Peace
 

Mkuu wa wilaya ya Hai akiangalia moja ya eneo la barabara ya Machame ambalo lina kasoro katika ukarabati wake huku maofisa wa Tanroads mkoa wa Kilimanjaro wakitoa maelezo
 

No comments:

Post a Comment