Uchangiaji huo unatarajia kufanyika Leo katika shule ya Sekondari Hai kuanzia saa tatu
kamili.
Mratibu wa chama cha msalaba mwekundu, kisaidizi
cha serikali (Red cross) wilaya ya Moshi David Sinda aliyasema hayo wakati
akizungumza na Redio Boma Hai kuhusiana
na suala la uchangiaji wa damu salama kwa hiari.
Sinda alisema uhaba wa damu katika benki ya damu
imekuwa chanzo cha wanawake wengi kupoteza maisha baada ya kujifungua kutokana
na kutokwa na damu nyingi huku wananchi wengi hawana utayari wa kuchangia damu.
“Tuwasaidie hawa wanawake wanaopoteza maisha baada
ya kujifungua kwa kushiriki kikamilifu katika zoezi la uchangiaji wa damu
salama kwa hiari ambalo linaloendelea hivi sasa”alisema Sinda
Kwa upande wake mratibu wa huduma za kutunza
wagonjwa majumbani mkoa wa Kilimanjaro Leticia Mwigamba alisema kuna uhitaji
mkubwa wa damu kwa wanawake, wazee na watoto ambao wameonekana kuathirika
zaidi.
Akizungumzia suala la baadhi ya watumishi kutokuwa
waaminifu na kuwauzia damu watu wenye uhitaji wa damu Mwigamba alisema ni vyema
wananchi wakatoa taarifa sehemu husika ili hatua zichukuliwe kukomesha hali
hiyo.
“Kuna baadhi ya wauguzi sio waaminifu wanawauzia
damu wagonjwa tunatoa wito kwa wananchi kutoa taarifa kwa sababu huduma ya damu
ni bure kwa wagonjwa hospitalini” alisema “Leo tunaendesha zoezi la uchangiaji wa damu
salama hapa wilayani Hai ikiwa ni katika kuelekea kwenye kilele cha maadhimisho
ya siku ya chama cha msalaba mwekundu ulimwenguni ambayo huadhimishwa kila
tarehe 8 may, ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni” my red cross story” na kitaifa
itafanyika Jijini Mbeya” Alisema Mwigamba
No comments:
Post a Comment