Kutokana na hatua hiyo Halmashauri ilikabidhiwa ngao ya Ushindi na
Kiasi cha shilingi milioni tano ikiwa ni motisha kwa Halmashauri ya Wilaya ya Hai
kuendelea kufanya vizuri na Halmashauri zingine kujifunza kutoka Hai.
Akikabidhi zawadi hizo mama Salama Kikwete amewataka wazazi, walezi na waalimu
kushirikiana katika kuhakikisha kuwa watoto wa kike wenye umri wa miaka tisa
hadi kumi na tatu wanapata chanjo ya saratani ya shingo ya kizazi.
Uzinduzi huo wa chanjo
hiyo ya majaribio ya shingo ya uzazi ulihudhuriwa na Naibu waziri wa
afya na ustawi wajamii Dk Kyebwe Stivine Kyebwe, Dk Sudha Sharma mwakilishi
toka UNICEF, Rufaro Chatora Mwakilishi toka shirika la afya duniani WHO pamoja
na viongozi wengine wakiserikali.
Mke wa raisi amewataka wazazi na walenzi kuondokana na
kasumba mbaya ya kusema kuwa chanjo hiyo itawafanya watoto kuwa wagumba na kusema kuwa chanjo hiyo ni salama
kiafya nchi za wenzetu wameweza kutokomeza saratani kwa chanjo ya HPV.
No comments:
Post a Comment