Friday, September 12, 2014

WANAFUNZI 4704 WAFANYA MTIHANI WA KUHITIMU ELIMU YA MSINGI WILAYANI HAI



Zaidi ya wanafunzi    4704 wamefanya  mtihani wa kuhitimu  darasa la saba  katika Wilaya ya Hai katiyo  wavulana  2347  na wasicha 2357. 

Akizungmza siku moja kabla ya mtihani huo kufanyika, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai ndugu Melkizedeck Humbe  amesema wanafunzi hao watafanya mtihani hiyo katika  vituo 21  ambavyo maandalizi yote yalikuwa yamekamilika na kupatiwa vifaa vyote.

Ndugu humbe aliwaagiza wasimamizi wa mitihani katika kusimamia mithani bila ya udanganyifu katika kusimamia mitihani hiyo na kuwataka kufuata taratibu za utumishi wa Umma.

Kwa upande mwingine alitoa wito kwa  wanafunzi wa darasa la saba kuondoa hofu na kutokuwa na wasiwasi  wakati wa kufanya mtihani huo,pia aliwataka wafanye mtihani hiyo kwa hali ya usafi ili kurahisisha usahishaji wa mitihani.


No comments:

Post a Comment