Tuesday, February 25, 2014

MKUU WA WILAYA YA HAI AOMBA WADAU WA MAENDELEO KUSAIDIA WALIOATHIRIKA NA MAAAFA

 MKUU WA WILAYA YA HAI AOMBA WADAU WA MAENDELEO KUSAIDIA WALIOATHIRIKA NA MAAAFA

Mkuu wa wilaya ya Hai Novatus Makunga akipokea msaada wa unga wa mahindi kutoka kwa mwakilishi wa kampuni ya Bonite

Mkuu wa wilaya ya Hai Novatus Makunga amewaomba wadau mbali mbali kuendelea kusaidia wananchi wa Wilaya ya Hai waliokumbwa na maafa yaliyosababishwa na upepo mkali ulioambatana na mvua na kuezua paa za kaya zaidi ya  200.


Mkuu wa wilaya alitoa wito huo wakati akipokea msaada wa kilo 2500 za unga wa mahindi, kilo 1000 za maharage na mabati 200 zilizotolewa na mwenyekiti wa makampuni ya IPP kupitia kampuni ya vinywaji baridi ya Bonite Bottlers ya Mjini Moshi.

Alisema miisaada bado inahitajika zaidi kwa walioathirika  hasa kwakuwa wananchi wameanza matayarisho ya kilimo kutokana na mvua ambazo zimeanza kunyesha na kusisitiza umuhimu wa misaada ya kibinadamu.

Ametaja wadau wengine waliotoa misaada kuwa ni pamoja na Chama Kikuu cha Ushirika Mkoani Kilimanjaro(KNCU) kupitia mwenyekiti wake Ndugu Menald Swai kilitoa msaada wa shilingi milioni moja, kampuni ya MONOBAN ya jijini Arusha iliyotoa tani nne za unga na shilingi milioni moja za kununulia maharage zilizokabidhiwa na  Mkurugenzi mkuu wa kampuni hiyo Ndugu Godfrey Mollel.

Misaada hiyo tayari imeshasambazwa katika kata za Machame Weruweru,Machame Kusini,Masama Rundugai,Masama Mashariki,Masama Magharibi na Masama Kati.



Wafanyakazi wa kampuni ya vinywaji baridi Bonite Bottlers wakishusha moja ya magunia ya chakula kilichotolewa kama msaada kusaidia waliopatwa na maafa


Mkuu wa wilaya ya Hai ndugu Novatus Makunga akipokea msaada wa mabati kutoka kwa mwakilishi wa bonite kwa ajili ya kusaidia watu waliokumbwa na maafa ya upepo



No comments:

Post a Comment