Monday, March 24, 2014

MAADHIMISHO YA WIKI YA MAJI WILAYA YA HAI YAFANA



Mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Hai Mh Clement Kwayu amewataka wananchi kutunza miradi iliyopo katika maeneo yao kwa faida yao na vizazi vijavyo.

Mh Kwayu aliyasema  hayo katika kata ya KIA wakati wa uzinduzi wa mradi wa maji unaoanza kutekelezwa katika vijiji vya kata hiyo  ikiwa pia ni mpango wa matokeo makubwa sasa ambapo pia mradi huo unategemea kugharimu zaidi ya shilingi bilioni tatu huku ukitarajiwa kukamilika mwezi  july mwaka huu.

‘Wananchi wanapaswa kutambu kuwa maji ni uhai  kwa kiumbe yeyote yule na kila mwananchi anao wajibu wa kulinda miundo mbinu hiyo maji ili huduma hiyo kupatikana kwa ukaribu na kwa wakati muafaka’alisema Mh Kwayu

Kwa upande mwingine Diwani wa kata ya KIA mh. Sinyoki pamoja na Mhandisi wa maji wa wilaya Nyakaraita Mwita  waliahidi  kushirikiana bega kwa bega kuhakikisha kuwa tatizo la maji katika ukanda wa tambarare linakwisha

Kwa upande mwingine Meneja wa Bodi ya maji Uroki Bomang’ombe Mhandisi Prosper Shoo aliwashauri wananchi wa Kijiji cha Kyeri kuifadhi mazingira kwa kupanda miti rafiki katika vyanzo vya maji  wakati wa ziara ya uhamasishaji wa upandaji miti katika  chanzo cha maji cha saaki katika maadhimisho ya wiki ya maji.

Shoo alisema kuwa kuna uharibifu mkubwa wa mazingira ambao unafanywa na wananchi hali iliyopelekea maji kupungua katika chanzo hicho cha saaki huku akiiomba jamii inayozunguka chanzo hicho kupanda miti ili kunusuru hali hiyo ambapo alisema awali chanzo hicho kilikuwa kinazalisha maji ujazo wa 42m³ kwa sekunde tofauti na sasa ambapo chanzo hicho uzalisha  ujazo wa 41m³  kwa sekunde.


No comments:

Post a Comment