Thursday, January 26, 2017

RC KILIMANJARO ASHAURI FEDHA ZA MIRADI ZIZINGATIE MAZINGIRA

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Meck Sadick akipokea taarifa ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na nyumba za walimu kwenye shule ya sekondari Kikafuu kutoka kwa Mkuu wa Shule hiyo. Wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Hai Gelasius Byakanwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Yohana Sintoo.                                      (Picha zote na Adrian Lyapembile)
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Meck Sadick akiongozana akitembelea jengo la darasa kwenye shule ya Sekondari KIA wilayani Hai lilijengwa kupitia mredi wa SEDEP

Jengo la vyumba vya madarasa kwenye shule ya sekondari KIA wilayani Hai lililojengwa kupitia mradi wa SEDEP

Jengo la choo cha walimu kwenye shule ya sekondari Kyuu wilayani Hai

Mhandisi Msangi wa wilaya ya Hai akitoa taarifa ya ujenzi wa vyoo kwenye shule ya sekondari Kyuu kwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Meck Sadick

Jengo la vyumba vya madarasa kwenye shule ya sekondari Kyuu lililojengwa kupitia mradi wa SEDEP

Baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari Kikafuu wilayani Hai iliyofaidika na ujenzi wa vyumba vya madarasa na nyumba ya walimu vilivyojengwa kupitia mradi wa SEDEP


Na Davis J. Minja
HAI - KILIMANJARO

MKUU wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Meck Sadick ameiomba serikali kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi pamoja na TAMISEMIi kuangalia upya gharama za ujenzi wa majengo katika miradi hasa mradi wa  SEDEP kuzingatia mazingira ya maeneo wanapopeleka mradi ili kiasi cha fedha kinachotolewa kiweze kutosheleza miradi hiyo.

Ametoa wito huo leo wakati wa ziara yake ya kutembelea takribani miradi minne katika shule za sekondari Wilayani Hai Mkoani humo kwa lengo la kukagua hatua zilizofikiwa katika miradi hiyo kwa fedha zilizo tolewa na serikali kwa ajili ya kuboresha huduma katika shule.

Sadick emezitaja shule zilizofaidika na mradi wa SEDEP kuwa ni pamoja shule ya sekondari KIA, shule ya sekondari Kyuu pamoja na shule ya sekondari Kikafuu ambapo kati ya shule hizo baadhi zimefanyiwa maboresho ya vyoo vya wanafunzi na waalimu na kuongezewa vyumba vya madarasa pamoja na nyumba za waalimu.

Hivyo ameishauri wizara kufanya maamuzi ya kuelekeza fedha hizo kwa halmashauri kutumia force akaunti ili kuweza kujenga majengo kwa gharama nafuu kwa kuwatumia wakandarasi wa wilaya kutokana na wakandarasi wanaopokea tenda kuwa na gharama kubwa huku kiasi kinachotolewa na wizara kuwa kidogo.

No comments:

Post a Comment