Friday, April 25, 2014

MKUU WA WILAYA YA HAI ASHUGHULIKIA TATIZO LA MBEGU KUTOOTA



Kufuatia  malalamiko ya  baadhi ya wakulima wa   Kijiji cha Kawaya Kata ya Masama Rundugai  ya kutoota kwa  mbegu za mahindi aina ya  SIDCO  513 na SIDCO  627 ambazo zilitolewa kwa ruzuku na   serikali , Serikali Wilayani Hai imeanza kufuatilia tatizo hilo kwa ukaribu ili kubaini chanzo chake.

Akizungumza katika Baraza la Halmashauri hivi karibuni, Mkuu wa Wilaya ya Hai ndugu Novatus Makunga  amesema tayari ameshawagiza   Maafisa Kilimo  ambao wameonana na wakala wa eneo husika na kuchukua sampuli  ambazo zitafanyiwa uchunguzi.

Amesema pia wamewasiliana na tawi la SICO Arusha ambao wamesema tayari wameshafanyia uchunguzi na kusema kuwa mbegu hizo ni bora lakini Serikali lazima ijiridhishe baada ya uchunguzi  unaofanywa na wakala wa mbegu Tengeru mkoani Arusha kukamilika.

Hata hivyo amesema  mbegu zinaweza kuacha kuota kutokana na kukaa kwa muda mrefu ardhini  na kukosa unyevu nyevu na baadaye kuoza au mbegu kokosa ubora suala ambalo litathibika baada ya uchunguzi kufanyika.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri Mh Clement Kwayu amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa hatua zilizochukuliwa na kumtaka aendelee kufuatalia suala hili kwa ukaribu zaidi.

Katika hatua nyingine Baraza hilo liliwaagiza wataalam wa Kilimo wa ngazi zote kuhakikisha kuwa wananchi wanapatiwa elimu ya kutosha juu uzuiaji wa viwavi jeshi ambavyo vinaripotiwa kuwa katika maeneo mbali mbali ya wilaya ya Hai na Mkoa wa Kilimanjaro kwa ujumla.

Akielezea hatua ambazo tayari zimechukuliwa Mkuu wa Idara ya Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika ndugu Lalashoi Kweka alisema tayari Idara imeshawasilisha taarifa katika ngazi mbali mbali ikiwa ni Mkoani na Wizarani na kuwasiliana na taasisi mbali mbali zinzofanya utafiti wa wadudu waharibifu wa mazao ambapo  serikali imetoa kiasi cha lita 80 za dawa aina ya Elthrin 25 EC lita 80  kwa ajili ya kasaidia familia zisizo na uwezo wa kununua dawa za kuangamiza viwavi jeshi.

Hata hivyo amesema juhudi bado zinafanyika za kuhamasisha na kuelimisha wananchii juu ya aina ya dawa zinazotakiwa kutumika kili kuangamaiza wadudu hao waharibifu na kwamba elimu hiyo imetolewa na wataalam kupitia kituo cha Redio Boma Hai FM kinacho milikiwa na Halmashauri na kwamba hali si mbaya sana kwani wananchi wengi wameshapiga dawa.

No comments:

Post a Comment