Maazimio ya kufukuzwa kazi kwa watendaji hao yamefikiwa baada ya Baraza hilo kujadili kwa muda mrefu na kujiridhisha juu ya taarifa iliyowasilishwa kwao juu kutoripoti kazini kwa watumishi hao ambao baadhi yao wamekwenda masomoni bila kufuata taratibu.
Akizungumza kwenye Baraza hilo Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Melkizedeki Humbe alisema watumishi hao wamefukuzwa kazi kwa kuzingatia sheria namba 57(1) kifungu kidogo cha kwanza kwamba mtumishi anapotoroka kazini kwa zaidi ya siku tano mfululizo bila taarifa anatakiwa kufukuzwa kazi.
Amesema kamati iliundwa kwa ajili ya uchunguzi na kuwapa nafasi ya kujitetea kwenye kamati ambapo kuna waliojitokeza na wengine hawakujitokeza na waliojitokeza pia utetezi wao haukukubalika ndipo umauzi huo wa kuwafukuza ulipofikiwa
No comments:
Post a Comment